Tanzania,Marekani zajadiliana fursa za uwekezaji Sekta ya Madini

DODOMA-Ujumbe wa watu sita kutoka nchini Marekani Julai 16, 2024 umekutana na Wataalam wa Wizara ya Madini na Taasisi zake na kujadiliana kuhusu ya fursa za uwekezaji zilizopo katika Sekta ya Madini.
Katika Mkutano huo, Timu ya upande wa Tanzania imeongozwa na Kamishna wa Madini Dkt. AbdulRahman Mwanga akiambatana na Kamishna Msaidizi wa Madini anayeshughulikia Ushiriki wa Watanzania katika Sekta ya Madini Maruvuko Msechu na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) Dkt Mussa Budeba.
Katika majadiliano hayo, GST imewasilisha mada juu ya fursa zilizopo kupitia taarifa za tafiti mbalimbali zilizofanyika hapa nchini ambapo Mjiolojia Mwandamizi kutoka GST Masota Magigita ameelezea kuhusu hali ya jiolojia ya Tanzania na uwepo wa madini kupitia tafiti zilizofanyika kwa njia ya Jiolojia , Jiofikia na Jiokemia.

Aidha, Magigita amefafanua kuwa katika taarifa za jiosayansi zilizopo zimebainisha aina mbalimbali za madini yakiwemo madini mkakati, madini ya metali, madini ya vito, madini ujenzi na madini adimu (REE).

Naye, Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini kutoka Tume ya Madini, Andrew Mgaya amesema kuwa Tanzania inaendelea na uzalishaji wa madini ya kinywe ambapo mwaka 2023/2024 kiasi cha tani 196,682.58 zilizalishwa kutoka tani 10,069.55 zilizozalishwa kwa mwaka wa 2022/2023.
Imependekezwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuendeleza sekta ya madini hususani madini mkakati na madini adimu katika maeneo makuu matatu ambayo ni kufanya utafiti katika maeneo yenye madini mkakati, ushirikiano wa kiufundi wa utekelezaji wa sheria na ushirikiano katika utekelezaji wa tafiti za Jiosayansi.
Awali, baada ya kupokea wasilisho la GST , Wakili Pencak aliipongeza wizara ya madini kwa kufanya tafiti mbalimbali za madini zinazovutia uwekezaji.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news