TARURA,TANROADS na WB wakagua mradi ujenzi Barabara ya Iringa hadi Kilolo

IRINGA-Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Mhandisi Victor Seff leo Julai 2,2024 ameshiriki katika ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa Barabara ya Iringa - Kilolo akiambatana na TANROADS na ujumbe wa Benki ya Dunia (WB).
Mradi huo ni sehemu ya Mradi wa uboreshaji wa barabara vijijini na ufunguaji wa fursa za kiuchumi na kijamii unaotekelezwa na TARURA na TANROADS.
Ujumbe huo wa Benki ya Dunia unatembelea Miradi ya RISE kuona kama utekelezaji wake unaendelea kulingana na Mpango wa utekelezaji uliokubalika na kuona changamoto katika utekelezaji kama zipo.
Mradi wa ujenzi wa barabara ya Iringa (Ipogolo)-Kilolo (33.61) ni wa kiwango cha lami unatekelezwa na Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) na Mkandarasi China Henan Engineering Company.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news