Temeke yaimarisha Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

DAR-Halmashauri ya Manispaa ya Temeke mkoani Dar es Salaam ambayo ni mshindi wa kwanza na wa jumla kwenye utoaji taarifa kwenye Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa, imenunua vitendea kazi vya shilingi milioni 78 kwa ajili ya Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.
Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Bw. Elihuruma Mabeyla amesema, kwa kutambua mchango wa Kitengo cha Habari Serikilini na kazi kubwa wanayoifanya Manispaa ya Temeke imefanya manunuzi ya vitendea kazi vya kisasa vyenye thamani ya shilingi milioni 78 kwa ajili ya maafisa habari wao.
"Temeke tumekuwa wa kwanza na tunataka kuendelea kubaki kwenye nafasi hii, hivyo vifaa hivi ni mbinu bora ya kujipanga kuendelea kutoa taarifa bora, sahihi na kwa wakati ili tuendelee kushikilia nafasi yetu na kuhabarisha umma kazi kubwa inayofanywa na Rais wetu Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news