VIDEO:TFRA yanadi fursa za uwekezaji viwanda vya ndani vya mbolea

Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) chini ya Wizara ya Kilimo imeanzishwa kwa Sheria ya Mbolea Na. 9 ya mwaka 2009.

Aidha,mwaka huu ni miongoni mwa taasisi za umma ambazo zinashiriki katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Sabasaba vilivyopo Halmashauri ya Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam.


MAJUKUMU YA TFRA

1. Kusimamia na kudhibiti ubora wa mbolea nchini.

  • Kusajili mbolea.
  • Kufanya ukaguzi wa ubora wa mbolea katika mnyororo wa tharnani.

2. Kudhibiti utengenezaji, uingizaji na biashara ya mbolea nchini.

  • Kusajili, kutoa leseni, na kutunza kumbukumbu za waten­genezaji na wauzaji wote wa mbolea.
  • Kutoa vibali vya watengenezaji, waagizaji, wasambazaji wa mbolea nchini na wauzaji wa mbolea nje ya nchi.
  • Kusimamia bei za mbolea nchini.
  • Kuunganisha wauzaji na wanunuzi wa mbolea nchini ili kuhakikisha kwamba mbolea inayotosheleza inapatikana kwa wakati.

3. Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa Serikali na taasisi zingine juu ya masuala yanayohusu sera za usimamizi na udhibiti wa ubora na biashara ya mbolea.

4. Kushirikiana na asasi za ndani na nje ya nchi zinazoshughu­likia mbolea katika kuhakikisha mbolea inamfikia mkulima katika ubora unaokubalika na bei nafuu.

5. Kushirikiana na Mamlaka za Serikali za Mitaa katika kuelimi­sha Umma juu ya matumizi sahihi ya mbolea.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news