Wataalam wa Kamati ya Mawaziri wa Fedha na Uwekezaji na Jopo la Uchumi Jumla SADC wakutana

DAR-Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban ameongoza ujumbe wa Serikali katika mkutano wa wataalam wa Kamati ya Mawaziri wa Fedha na Uwekezaji na Jopo la Uchumi Jumla wa nchi zilizopo katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ulionza tarehe 29 hadi 31 Julai 2024. Mikutano hii itajadili masuala mbalimbali ikiwemo uanzishwaji wa mfuko wa kifedha wa kanda, kujadili taarifa ya tathmini ya hali ya uchumi kwa nchi wanachama ikiwemo Tanzania, taarifa ya mgombea atakayeiwakilisha SADC katika uchaguzi wa nafasi ya Rais wa AfDB, kupokea na kujadii taarifa mbalimbali za kamati ndogo zilicho chini ya SADC.
Katika mikutano hii inayofanyika katika ofisi za Makao Makuu Ndogo za Benki Kuu jijini Dar es Salaam, ujumbe wa Tanzania unaoshiriki katika mkutano huu, unajumuisha wawakilishi kutoka Wizara ya Fedha, Wizara ya Mipango na Uwekezaji, Wizara ya Mambo ya Nje, Tume ya Mipango, Benki Kuu ya Tanzania, Mamlaka ya Masoko na Mitaji na Dhamana (CMSA), Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu (FIU) na Benki ya Maendeleo TIB.
Mikutano hii itafuatiwa na mkutano wa Mawaziri wa Fedha na Uwekezaji na Magavana wa Benki Kuu za nchi wanachama wa SADC tarehe 6 na7 Agosti 2024.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news