Waziri Kairuki ateta na Mkurugenzi wa UN Tourism

LUSAKA-Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani (UN Tourism) Kanda ya Afrika, Bi. Elcia Grandcourt.
Pamoja na mambo mengine kikao hicho kilijikita katika kuendeleza ushirikiano na Shirika hilo hususan, fursa na programu mbalimbali za chombo hicho katika maeneo ya uendelezaji wa mazao ya utalii, utangazaji utalii, kuvutia uwekezaji katika miundombinu ya utalii na huduma, utoaji wa mafunzo na kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya utalii.
Kikao hicho kilimefanyika leo katika Hoteli ya Avani Victoria Falls Resort, Jijini Livingstone Zambia na kuhudhuriwa na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kitaalam wa UN, Bw. Jaime Mayaki, Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Utalii, Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Richie Wandwi pamoja na Afisa Utalii wa UN Tourism, Bi. Zineb Remmal.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news