Waziri Mkuu akagua ujenzi Mnara wa Mashujaa

DODOMA-Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Julai 12, 2024 amekagua ujenzi wa Mnara wa Mashujaa uliopo mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma ikiwa ni maandalizi ya Siku ya Mashujaa itakayofanyika Dodoma, Julai 25, 2024.

Akizungumza baada ya kufanya ukaguzi wa mnara huo Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi na amemtaka mkandarasi wa mnara huo ambaye ni Suma JKT kukamilisha ujenzi kwa viwango na ubora ifikapo Julai 22, mwaka huu.
Naye, mshauri elekezi kiongozi, Dkt. Ladislaus Mrema amesema kuwa awamu ya kwanza ya ujenzi wa eneo hilo la mnara unajumuisha ujenzi wa uwanja wa gwaride, ngazi, njia za watu wenye mahitaji maalum pamoja na kitako cha mnara na bushati eneo la kuzunguka mnara. “Mpaka sasa mradi huu umefikia asilimia 84.”
Siku ya Mashujaa itafanyika Julai 25, mwaka huu na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news