Waziri Ndejembi ataka uadilifu na kutenda haki kwa watumishi wa Sekta ya Ardhi

DAR-Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Mhe. Deogratius Ndejembi amewataka watumishi wa sekta ya ardhi nchini kuongeza uadilifu na kutenda haki katika utekelezaji wa majukumu yao sambamba na kuongeza kasi katika utendaji kazi.
Mhe. Ndejembi namesema, suala la ardhi ni gumu na linahitaji watumishi kuwa makini ambapo amesisitiza kuwa ni lazima watumishi wa sekta ya ardhi watende haki huku wakizingatia kuwa kuna sheria, kanuni na miongozo inayowaoongoza katika utendaji kazi.
Aidha, Mhe. Ndejembi amesema, yale yote mazuri yaliyofanywa na mtangulizi wake ikiwemo Kliniki za Ardhi atayaendendeleza kwa lengo la kuleta ufanisi wa wizara.

‘’Sikuja kutengua torati, yote aliyoyaanzisha mtangulizi wangu ikiwemo kliniki za ardhi zitaendelea na vile vile anayehisi jambo lake limekwama ajitokeze na atahudumiwa,’’ amesema Mhe. Ndejembi.
Mhe. Ndejembi ametoa kauli hiyo tarehe 26 Julai 2024 wakati akizungumza na viongozi pamoja na watumishi wa Wizara ya Ardhi mkoa wa Dar es Salaam mara baada ya kutoka kuapishwa kushika nafasi hiyo kutoka kwa mtangulizi wake Mhe. Jerry Silaa.

Sambamba na hayo Waziri huyo wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ametaka kuimarishwa kwa mifumo ndani ya wizara ili migogoro ya ardhi isiendelee kujitokeza.
Mhe. Ndejembi ameapishwa na Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kuwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi akitokea Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news