Wizara ya Elimu yajifunza jambo Afrika Kusini, yatoa ahadi

PRETORIA-Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo na wataalamu wa elimu kutoka Tanzania Bara na Zanzibar wameshiriki kikao cha pamoja na Wizara ya ElimuMsingi ya Afrika Kusini ambapo ameipongeza wizara hiyo kwa jitihada kubwa wanazozifanya katika sekta ya elimu.
Kikao hicho kimefanyika Julai 19, 2024 katika ofisi za Wizara ya ElimuMsingi jijini Pretoria nchini Afrika Kusini, Prof. Nombo amezitaja jitihada hizo ni pamoja na Serikali kuweka bajeti toshelevu kwa Wizara ya Elimu na kuwezesha mwanafunzi katika shule kupatiwa vitabu vya masomo yote pamoja na chakula.
Prof. Nombo ameongeza kuwa Tanzania katika masuala hayo imejifunza na kwamba serikali itaona namna ya kuimarisha eneo hilo ili kuongeza ufanisi wa ufundishaji, ujifunzaji na upimaji wa wanafunzi shuleni.

Aidha, Prof. Nombo ameiahidi Afrika Kusini kuipatia msaada wa kitaalamu kutoka Tanzania katika tathmini ya mtaala na vifaa vyake kwa ajili ya kufundishia somo la Kiswahili katika shule nchini humo.
Sambamba na hilo, alitoa vitabu mbalimbali vya Kiswahili zikiwemo Kamusi, vitabu vya kufundishia Kiswahili kwa wageni, mitaala, mihutasari ya somo pamoja na vitabu vya taarifa za tathmini ya ufaulu wa watahiniwa kwa somo la Kiswahili.

Katibu Mkuu amesema, utoaji wa vitabu hivyo ni hatua za awali za kuchochea ufundishaji na ubidhaishaji wa lugha ya Kiswahili nchini humo.
Pia, Prof. Nombo aliahidi kuwa Tanzania itaendelea kuimarisha ubidhaishaji wa Kiswahili kwa njia mbalimbali ikiwemo mitandao ili kuwavutia na kuwashawishi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news