LONDON-Sekta ya Utalii Tanzania inatarajiwa kuchangia robo tatu ya Bajeti Kuu ya Serikali ya sasa ifikapo mwaka 2034.

Ni ripoti iliyotolewa Juni 26, 2024 jijini London nchini Uingereza ambayo inaonesha Tanzania kuwa, moja ya mataifa ambayo yameendelea kunufaika kiuchumi na mageuzi makubwa yanayoendelea nchini chini ya Rais wa Awamu ya Sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Sekta ya Utalii.

Aidha,kiasi kilichotumiwa na watalii kwa huduma mbalimbali (visitor spending levels) kimepanda mwaka jana 2023 na kuweka rekodi ya juu zaidi ambapo watalii wa nje walitumia shilingi trilioni 8 huku wa ndani wakitumia shilingi trilioni 3.7 sawa na ongezeko la asilimia 11.1 na 12.8 mtawalia ikilinganishwa na mwaka 2019.
Ripoti hiyo pia inaonesha kuwa, ajira katika sekta ya utalii Tanzania mwaka 2023 zilifikia watu milioni 1.4 ikiwa ni ongezeko la ajira 97,000 lakini zikiwa pungufu kidogo kwa asilimia 7.4 ikilinganishwa na rekodi ya juu mwaka 2019.

“Sekta ya Utalii ya Tanzania inazidi kuimarika kila uchao ikiweka rekodi za juu kuwahi kufikiwa,” anasema Mtendaji Mkuu wa WTTC Julia Simpson kuhusu ripoti ya Tanzania.
Aidha, Tanzania ni miongoni mwa nchi chache za Afrika ambazo mafanikio yake yamechambuliwa kwa kina katika tovuti ya baraza hilo. Soma hapa》》》
