Azam FC yakiri kulitia Taifa aibu

DAR-Afisa Habari wa Azam FC, Hasheem Ibwe amekiri timu hiyo kulitia aibu Taifa, kwani ilikuwa ikitarajiwa kuibuka na ushindi mnono.

Ameyasema hayo baada ya matajiri hao wa Jiji kutolewa kwenye mashindano ya Klabu Bingwa barani Afrika hatua ya mtoano kwa kufungwa mabao 3-1 kwa matokeo ya jumla na APR ya Rwanda.
"Tumewaangusha mashabiki wetu, tumewaangusha Watanzania wote tumekuwa aibu kwenye Taifa la watu mbele ya timu ambayo tunaiweza, mbele ya timu ambayo tungeweza kupata ushindi nyumbani na ugenini.

"Hatujacheza vizuri hata kidogo mechi zote mbili kuna wakati lazima ukweli mchungu useme tumefedheheka mno. Timu yetu sio mbaya ina ubora wa hali ya juu, lakini tumeondoshwa ugenini.

"Siombi Msamaha leo wala sitetei WE NEED CHANGES ,WE NEED TO CHANGE, Soon Mtafurahi, Azam Itacheza tena ,Azam Itafunga sana Azam Itakuwa Tishio RED BUTTON ON".

Timu hiyo imetolewa kwenye michuano hiyo baada kukubali kipigo cha mabao 2-0 ugenini nchini Rwanda na kutoka na ushindi wa bao 1-0 nyumbani katika mchezo wa awali.

Timu ya Yanga pekee ndio imebakia kuwakilisha Tanzania kwenye michuano hiyo mikubwa barani Afrika baada kushinda mabao 10 - 0 dhidi ya Vital’O ya Burundi kwa michezo miwili iliyochezwa katika dimba la Azam Complex, Chamazi mkoani Dar es Salaam.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news