Balozi Nchimbi ampa kongole Mbunge Mama Salma Kikwete kwa kazi nzuri Mchinga

LINDI-Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Balozi Dkt.Emmanuel Nchimbi amepokea taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi katika Jimbo la Mchinga mkoani Lindi huku alimpongeza Mbunge wa jimbo hilo, Mama Salma Kikwete kwa kazi nzuri.
"Niseme nimeisikiliza taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM, tena kwa umakini sana kwa niaba ya CCM nakupongeza wewe na viongozi wenzako kwa kazi kubwa unayofanya. Umetembelea kata zote na vijiji vyote.
"Umetumia hadi bodaboda na bajaji kuwafikia wananchi wa Jimbo la Mchinga, unaguswa na changamoto za wananchi wenzako wa Mchinga na unapambana kutatua kero zao kwa kuzisemea Bungeni na kuwaomba mawaziri kufika huku wao wenyewe.”

“Wakati wanatazama ile video ya uwasilishaji wa taarifa hiyo ya utekelezaji wa ilani, kuna mama mmoja amesema hakutegemea kwa hadhi yako ulivyo, kwamba ungeweza kulizunguka jimbo zima la Mchinga.

"Mimi pamoja na wenzangu Wajumbe wa Sekretarieti tumefurahishwa sana ya utekelezaji huu mzuri wa Ilani ya CCM ya Uchaguzi 2020/2025, ndani ya miaka hii mitatu. Tunakutakia kila la heri katika kumalizia hayo mengine yaliyobakia katika kukamilisha Ilani ya 2020 - 2025.”
Naye Mbunge wa Jimbo la Mchinga Mhe. Salma Rashid Kikwete wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020/2025, amepongeza Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya kwenye nchi yetu ya Tanzania, pamoja na Jimbo la Mchinga, ambapo hadi sasa ambapo takriban Sh. 18.4 bilioni zimetumika katika Sekta ya Elimu ikiwemo kujengwa Shule ya Wasichana ya Mkoa wa Lindi Mchepuo wa Sayansi, iliyojengwa katika Kijiji cha Kilangala huku uboreshaji wa huduma za afya ukifanyika kwa mafanikio makubwa na umeme tayari umefika katika vijiji vyote jimbo zima, sasa unaanza kuunganishwa kwenye vitongoji.
Baada ya kuwasilisha taarifa hiyo Julai 31,2024, Mama Salma Kikwete amekabidhi pikipiki kwa Polisi Jamii wa Jimbo la Mchinga na shule za sekondari katika kata zote za jimbo hilo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news