Bodi ya Mikopo yatoa taarifa muhimu kwa wanafunzi wa Stashahada (Diploma)

1. Kuanzia mwaka wa masomo 2023/2024 Serikali ilianza kutoka mikopo kwa wanafunzi wenye sifa wanasoma stashahada (Diploma) za kipaumbele kwa Taifa ambazo zinatajwa kwa kina katika ‘Mwongozo wa Utoaji Mikopo kwa Stashahada kwa 2024/2025’ unaopatikana katika heslb.go.tz;

2.Hivyo, katika mwaka wa masomo 2024/2025 unaotarajiwa kuanza mwezi Oktoba, 2024, wanafunzi wenye sifa wanaendelea kuomba ili hatimaye kuwezeshwa kusoma kozi za stashahada;

3. Kwa kuwa dirisha la kuomba mikopo kwa njia ya mtandao linakaribia kufungwa, (Agosti 31, 2024) tunawakumbusha kuwa stashahada zinazopewa kipaumbele ni kwenye maeneo yafuatayo:

a. Health and Allied Sciences

b. Education and Vocational Training

c. Transport and Logistics

d. Energy Engineering, Mining and Earth Science

e. Agriculture and Livestock

f. Kozi nyinginezo
‘Energy Engineering’, ‘Mining & Earth Science’, na ‘Agriculture & Livestock’ ambazo hazikutajwa kwenye kipengele cha D na E kama tangazo linavyoonesha, wanaruhusiwa kuomba mkopo na watapimwa uhitaji wao wa mkopo kupitia kingámua uwezo.

KUMBUKA: Ili kuomba mkopo, tembelea: olas.heslb.go.tz/olams/pre-appl…

Imetolewa na:
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
Jumatano, Agosti 28, 2024

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news