Bosi wa TIC atembelea Mradi wa AvoAfrica mjini Makambako

NJOMBE-Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Gilead Teri amefanya ziara mkoani Njombe na kutembelea mradi wa AvoAfrica mjini Makambako.
AvoAfrica, mwekezaji mkubwa katika usindikaji wa parachichi, sasa inapanua uwekezaji kwa kujenga kiwanda cha kusindika mafuta ya parachichi.

Kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kusindika tani 100,000 za parachichi kwa mwaka. Mashine zinatarajiwa kufika mwezi Novemba mwaka huu.
Uwekezaji huu, wenye thamani ya dola za Kimarekani milioni 4 utaongeza uzalishaji, kuboresha uchumi wa eneo, na mpaka sasa umezalisha ajira 180.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news