BoT yawapa mafunzo wanafunzi wa John Merlini Secondary

DODOMA-Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa mafunzo kuhusu kazi zake kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari John Merlini walipofanya ziara katika ofisi za makao makuu ya BoT jijini Dodoma. Katika ziara hiyo, wanafunzi wamepata fursa ya kujifunza kuhusu majukumu ya BoT katika kusimamia sera ya fedha, kudhibiti kiwango cha mfumuko wa bei, na kuhakikisha uthabiti wa uchumi wa nchi.
Vilevile, wanafunzi hao wamepewa elimu kuhusu alama za usalama zinazowezesha kutambua noti halali za Tanzania pamoja na njia sahihi za utunzaji wa noti na sarafu ili kuhakikisha zinaendelea kudumu katika mzunguko wa fedha kwa muda mrefu.
Mafunzo hayo yameendeshwa na Mchumi kutoka Tawi la BoT Dodoma, Bi. Regina Mwaipopo pamoja na Afisa Mwandamizi wa Benki, Bw. Atufigwege Mwakabalula.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news