Chini ya viti 3,000 huo uwanja hautatumika michezo ya Ligi Kuu

DAR-Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi ya NBC Tanzania, Almas Kasongo amesema, baadhi ya kanuni za ligi msimu ujao wa 2024/25 ni kuwa uwanja ambao hautakuwa na viti 3,000 kwa ajili ya mashabiki hautatumika kwenye michezo ya Ligi Kuu.
Ameyasema hayo leo Agosti 6, 2024 kwenye semina ya waandishi wa habari iliyosimamiwa na bodi hiyo jijini Dar es Salaam.

Kasongo amesisitiza kuwa, viti 3,000 ndio itakuwa idadi ya chini kabisa ya viti kwenye jukwaa, huku likitakiwa eneo la kuchezea na vyumba vya kubadilishia nguo ambavyo vinakidhi viwango.

Pia ameongeza kuwa, kanuni zinazitaka klabu kuwa na wachezaji wasiopungua wawili kutoka timu za vijana watakao kuwa sehemu ya mchezo katika mechi za ligi kuu nchini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news