Dkt.Isaka:Sitavumilia udanganyifu

DODOMA-Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima (NHIF), Dkt.Irene Isaka ameripoti rasmi katika Ofisi za Makao Makuu jijini Dodoma leo Agosti 19,2024.
Akizungumza na Menejimenti ya Mfuko na Watumishi, ameeleza jinsi ambavyo Serikali ilivyo na matarajio makubwa hasa katika utatuzi wa kero za wananchi kuhusu Bima ya Afya.
Ameahidi kutoa ushirikiano na amewataka watumishi kufanya kazi kwa ari, weledi, na uaminifu.
"Mimi nitakuwa kama Mama kwenu, lakini sina uvumilivu hata kidogo katika masuala ya udanganyifu na wasiowajibika katika majukumu yao, hivyo fanyeni kazi kwa bidii na kwa uadilifu pamoja na kunisaidia ili nitimize imani hii niliyopewa," amesema Dkt. Isaka.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news