Gharama za uendeshaji miradi kupatiwa unafuu Zanzibar-Rais Dkt.Mwinyi

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali ipo tayari kushirikiana na Taasisi za Mabenki Yasiyo na Mipaka (Bankers Without Boundaries) kuwekeza miradi ya kipaumbele na yenye tija kwa nchi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Mkuu wa Taasisi ya Mabenki Yasiyo na Mipaka ambayo Makao Makuu yake yapo nchini Uingereza, Bw. Matteo Scollabrino aliyefika Ikulu na ujumbe wake leo Agosti 14, 2024.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe: 14 Agosti 2024, alipokutana na Mkuu wa Taasisi ya Mabenki Yasiyo na Mipaka ambayo Makao Makuu yake yapo nchini Uingereza, Bw. Matteo Scollabrino aliyefika Ikulu na ujumbe wake.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Mkuu wa Taasisi ya Mabenki Yasiyo na Mipaka ambayo Makao Makuu yake yapo nchini Uingereza, Bw. Matteo Scollabrino aliyefika Ikulu na ujumbe wake leo Agosti 14, 2024.
Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesema sekta ya Uchumi wa Buluu, Kilimo, Nishati, Miundombinu, na Afya ni sehemu ya miradi ya kipaumbele kwa Serikali na inahitaji msukumo wa ziada ili iweze kuleta tija kwa nchi.
Naye Mkuu wa Bankers Without Boundaries, Bw. Matteo Scollabrino, amesema taasisi hiyo ambayo imeingia nchi 40 duniani inalenga kushirikiana na Serikali kwa kuwekeza katika miradi isiyo na athari za kimazingira pamoja na kupunguza mzigo wa gharama za uendeshaji na tayari imetenga kiasi cha Dola Milioni 500 kwa kufanikisha azma hiyo.
Kikao hicho ambacho kimefanyika Ikulu Zanzibar kimehudhuriwa na watendaji wa Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango na Presidential Delivery Bureau (PDB).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news