GEITA-Serikali imesema itaupatia Mji mdogo wa Katoro Mkoa wa Geita Wilaya ya Kipolisi na kuujengea Kituo kipya cha Polisi chenye hadhi ya Wilaya ili kuimarisha Ulinzi na Usalama wa raia na mali zao.

Naibu Waziri Sillo, amesema sababu za kupeleka hitajio hilo ni kutokana na Mji wa Katoro wenye watu zaidi ya laki tatu kukua kibiashara na kiuchumi kwa kasi.
"Kituo cha Polisi kilichopo kipo katikati ya makazi ya watu na maeneo ya biashara habari njema ni kwamba IGP alituma timu yake hapa walishafanya tathimini hivyo mnajengewa Kituo kipya cha kisasa na mnapatiwa Wilaya ya Kipolisi hapa Katoro."

Tags
Daniel Sillo
Jeshi la Polisi Tanzania
Wilaya ya Kipolisi Katoro
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi