Mabanda ya TMA yawa kivutio kwa wananchi Maonesho ya Nanenane

DODOMA,ZANZIBAR-Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imewakaribisha wananchi katika mabanda yao yaliyopo katika Maonesho ya Kitaifa ya Kilimo Nanenane yanayoendelea viwanja vya Nzunguni jijini Dodoma na viwanja vya Dole, Kizimbani jijini Zanzibar ili kupata elimu na kufahamu huduma wanazotoa kwa ustawi wa jamii na taifa kwa ujumla.
Wataalamu kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) wakiendelea kutoa elimu kwa wananchi katika viwanja vya Dole, Kizimbani, Zanzibar.
Wataalamu mbalimbali kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) wakiendelea kutoa elimu kwa wananchi katika viwanja vya NaneNane, Nzuguni, Dodoma.
Ikumbukwe kuwa, TMA ni mdau mkubwa katika sekta ya kilimo na mifugo nchini kwani, taarifa za hali ya hewa kilimo ni muhimu sana kwenye mipango na shughuli mbalimbali kwa mfano umwagiliaji ili kuhifadhi maji au nishati, kuchagua wakati unaofaa wa kutumia viuatilifu, matumizi ya mbolea, uzalishaji wa mifugo au uvuvi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news