Magazeti leo Agosti 13,2024

GEITA-Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Balozi Dkt.Emmanuel Nchimbi amemuagiza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mheshimiwa Daniel Sillo kuwaachia huru viongozi wote wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wanaoshikiliwa na polisi jijini Mbeya.

Balozi Nchimbi ametoa agizo hilo Agosti 12,2024 katika mkutano uliofanyika wilayani Geita wakati akizungumza na wakazi wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katoro, Geita ambapo ameuelekeza Naibu Waziri Sillo kuzungumza na Waziri wa Mambo ya Ndani ili viongozi hao wa CHADEMA waachiwe huru.
"Kwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani upo hapa, mambo ya sheria sio ya kutolea maelekezo Kiongozi wa chama cha siasa, lakini nitumie nafasi hii mwambie Waziri wako kwamba tunaomba muone uwezekano wale viongozi wa vyama vya siasa waachiliwe ili mtupe nafasi ya kuzungumza nao.


"Kwa sababu tunajenga Taifa moja tunapenda kuwa na Taifa tulivu kama kuna maeneo wamekosea wao au tumekosea sisi tukae tuzungumze tuijenge nchi yetu."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news