Magazeti leo Agosti 18,2024

DAR-Mfanyakazi wa Kampuni ya Mabasi ya Japanese katika Kituo cha Mabasi cha Kimataifa cha Magufuli (Mbezi Magufuli Bus Terminal) aitwaye Atukuzwe Nyato ametoweka nyumbani kwake katika mazingira ya kutatanisha tangu Jumapili ya Agosti 11, 2024 alipoaga kwenda kununua dawa na sasa familia yake inamtafuta na kuomba msaada kwa yeyote mwenye taarifa zake.



Aliaga nyumbani akiwa amevaa gauni la rangi ya njano na nyeusi ambapo ndugu zake wamesema alitoweka akiwa maeneo ya Kibanda cha Mkaa Mbezi huku marafiki, ndugu na wafanyakazi wenzake wa kampuni ya Mabasi ya Japanese wameendelea na jitihada za kumtafuta katika maeneo mbalimbali hadi sasa bila mafanikio.
Familia yake imefungua jalada la uchunguzi na kutoa taarifa katika vituo vitatu tofauti vya Polisi, Kituo kidogo cha Polisi cha Magufuli, Kituo cha Polisi Gogoni Mbezi na Oysterbay na inaomba msaada kwa mtu yeyote mwenye taarifa zake azipeleke kwenye Kituo chochote cha Polisi kilicho karibu nae au apige kwenye 0759246698 Rehema Muoka (Dada) au kwa 0654350406 Johson Mvena (Mfanyakazi Mwenzake).






Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news