Magazeti leo Agosti 4,2024

MANYARA-Wafugaji wanaoishi ndani ya eneo la Hifadhi ya Jamii ya Wanyamapori ya Burunge (Burunge WMA) wilayani Babati Mkoa Manyara na jirani na maeneo hayo, wamejengewa mazizi ya waya (boma hai) ili kuzuia wanyama wakali hasa simba na fisi kuvamia na kula mifugo nyakati za usiku.
Mazizi hayo yamejengwa na Taasisi ya Uhifadhi na Utalii ya Chem Chem, ambayo inafanya shughuli za uhifadhi na utalii katika eneo hilo, lilipo kati kati ya hifadhi ya Taifa ya Tarangire na Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara ikiwa ni sehemu ya mkakati wa taasisi hiyo, kupunguza migogoro baina ya wanyamapori na mifugo.
Akizungumza wakati wa kukabidhi mazizi hayo, Mkuu wa Wilaya ya Babati Mkoa wa Manyara, Lazaro Twange amesema,mradi wa ujenzi mazizi hayo ni utekelezaji wa maagizo ya Serikali kupunguza migogoro baina ya wanyamapori na binadamu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news