Magazeti leo Agosti 7,2024

LONDON-Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uingereza,Mheshimiwa Mbelwa Kairuki amesema kuanzia juzi kuna ujumbe mfupi wa video uliozunguka katika mitandao ya kijamii uliorekodiwa na raia wa Uingereza mwenye asili ya Tanzania,Martina Farrall, akielezea maisha yake kuwa hatarini huko anapoishi Ireland ya Kaskazini.  
Kwa mujibu wa taarifa aliyoitoa Agosti 6,2024 Balozi Kairuki amesema kufuatia ujumbe huo, Ubalozi umewasilisha taarifa ya Martina kwa mamlaka za Uingereza na kuomba hatua za kufuatilia suala hilo zichukuliwe mapema iwezekanavyo ili kuhakikisha usalama wake sambamba na kufanyia kazi tuhuma alizotoa ili kubaini ukweli wake na hatua kuchukuliwa.

“Aidha, leo tarehe 6 Agosti 2024 Afisa Ubalozi wa Tanzania anakwenda Ireland ya Kaskazini katika Mji anapoishi Bi. Farrall ili kukutana na mamlaka zinazohusika kufuatilia suala hilo.”

















Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news