Mifumo ya Elimu kusomana kuanzia awali hadi elimu ya juu

DODOMA-Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolf Mkenda, Naibu Waziri Mhe. Omari Kipanga, Katibu Mkuu Prof. Carolyne Nombo na Naibu Katibu Dkt. Franklin Rwezamula wamekutana na Menejimenti ya Wizara, Viongozi wa Taasisi na Makamu wakuu wa Vyuo Vikuu kujadili utekelezaji wa vipaumbele pamoja na utekelezaji wa Sera na Mitaala mpya.
Akizungumza katika kikao hicho Prof. Mkenda amesema kuwa wizara ipo katika mchakato wa kuunganisha mifumo ya elimu iweze kuongea kwa pamoja.
Waziri huyo ameongeza kuwa lengo ni kuona mifumo hiyo inawezesha kumfuatilia mwanafunzi kuanzia anapoanza elimu ya awali mpaka anapofika elimu ya juu na hata kama atakuwa amekwenda katika mfumo mwingine wa elimu ambapo kwa sasa ni ngumu kufata taarifa sahihi za wanafunzi katika ngazi mbalimbali.
"Kwa kweli kuna umuhimu wa kuwa na mifumo inayosomana na kuzungumza pamoja hii itatuwezesha kupata takwimu sahihi za wanafunzi ili tujue walipo wanafunzi hata kama watakwenda kwenye mfumo wa Cambridge," amesema Waziri.

Aidha, Prof. Mkenda amesema ni muhimu kwa Vyuo Vikuu vinavyojenga kampasi mpya katika mikoa mbalimbali kuwa na programu za kutoa shahada za amali badala ya kutoa taaluma ambazo tayari zipo katika vyuo hivyo.
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo amesema kuwa kikao hicho kinalenga kufanya tafakari ya masuala mbalimbali na vipaumbele ambavyo wizara imejipangia na namna inavyotekelezwa ili kuhakikisha mageuzi ya elimu yanatekelezwa ipasavyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news