Mtumishi wa SUMAJKT hatiani kwa kuomba na kupokea rushwa Tunduma

RUVUMA-Mahakama ya Wilaya ya Momba mkoani Ruvuma imemhukumu, Bw.Esau Andrew Hinjo aliyekuwa Askari wa SUMA JKT-Tunduma adhabu ya kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya shilingi 500,000.
Ni kwa kosa la kuomba na kupokea hongo Kinyume na Kifungu cha 15(1) (a) na 2 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura 329 Marejeo ya Mwaka 2022.

Hukumu dhidi ya Esau Andrew Hinjo imetolewa katika Kesi ya rushwa Na.23763/2024 leo Agosti 21, 2024 mbele ya Hakimu Mkazi,Mheshimiwa Claud Msenjelwa wa Mahakama ya Wilaya ya Momba.

Kesi hiyo imeendeshwa na Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU), Bi.Lilian Matara.

Ilielezwa kuwa,mshtakiwa alifikishwa mahakamani kwa shtaka la kupokea hongo kiasi cha sh.120,000 toka kwa Joseph Itera Chunche kama kishawishi cha yeye kutokamata nyavu haramu za kuvulia samaki. Mshtakiwa alikiri makosa yake na kulipa faini ya sh.500,000.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news