DODOMA-Mheshimiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Hamza Johari amewataka Menejimenti na Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kufanya kazi kwa bidii huku wakiifuata na kuiishi kauli mbiu ya ofisi hiyo ya Weledi na Ubora.



Mwanasheria Mkuu wa Serikali ameahidi ushirikiano wa kutosha kwa Menejimenti na Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika kufanikisha utelekezaji wa majukumu yao.


Awali, akiwakaribisha Viongozi hao wapya katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi amewapongeza Viongozi hao kwa kupata uteuzi huo na kuwaahidi ushirikiano kwenye masuala mbalimbali kila itakapohitajika.
Pia, ameitaka Menejimenti ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kuwapa ushirikiano Viongozi hao wapya walioingia katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

"Katika hatua nyingine aliyekuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ambaye sasa ni Mshauri wa Rais, Sheria na Mikataba Balozi Prof. Kennedy Gastorn akizungumza wakati wa hafla hiyo, aliwakaribisha Mwanasheria Mkuu na Naibu Mwanasheria Mkuu katika Ofisi huku akiiomba menejimenti ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuendelea kutoa ushirikiano kwa Viongozi wapya kama ambavyo walikuwa wakifanya chini ya uongozi uliopita.

Naye Mwandishi Mkuu wa Sheria Bw. Onorius Njole, akizungumza kwa niaba ya Menejimenti ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, amewapongeza na kuwakaribisha viongozi wapya kwa kuajidi kuwa menejimenti itatoa ushirikiano na pia akiwashukuru na kuwatakia kila kheri kwenye majukumu yao mapya viongozi wanaondoka kwa utumishi wao ndani ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
“Kwa niaba ya Menejimenti ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali nawakaribisha sana Viongozi wetu wapya kwenye Ofisi hii na mimi na wenzagu tunawaahidi kuwapa ushirikiano wa kutosha wakati wa kutekeleza majukumu yenu.

Baada ya kikao hicho Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali walikabidhiwa nyaraka na watangulizi wao, na kupata nafasi ya kutembelea Ofisi.
Tags
Habari
Hamza Johari
Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Weledi na Ubora
Wizara ya Katiba na Sheria