ADDIS BABA-Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu -Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi ameshiriki katika Mkutano wa Umoja wa Afrika wa Kamati ya Kitaalam wa Mawaziri wa Afrika wanaoshughulikia masuala ya maendeleo ya jamii, kazi na ajira uliofanyika Agosti 1, 2024 jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Aidha, Mkutano huo hufanyika kila baada ya miaka miwili ambapo kwa mwaka huu 2024 mkutano huo umeongozwa na kauli mbiu isemayo, "Kudumisha Maendeleo Jumuishi katika Jamii yote.”




Mkutano huo umeudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mwanaidi Khamis pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Zuhura Yunus Abdallah.