NA VERONICA MWAFISI
NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu amewaasa Watumishi wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kuwajibika kwa viwango vikubwa katika kutekeleza majukumu yao ili kutimiza azma ya taasisi hiyo katika kutoa ajira kwa kutenda haki sawa kwa kila mwananchi.

