OUT kutoa elimu juu ya huduma za chuo katika Maonesho ya Nanenane

DODOMA-Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kutumia fursa ya Maonesho ya Nanenane yanayoendelea Kitaifa mkoani Dodoma kutoa elimu kwa wadau mbalimbali wanaotembelea banda la chuo katika maonesho haya.
Akizungumza katika maonesho haya Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko Dkt. Adam Namamba amesema “Banda letu la Maonesho limejizatiti vizuri na huduma za udahili katika programu za chuo ngazi zote vilevile watumishi wetu wa OUT wanaendelea na kazi ya uelimishaji kwenye maonesho haya huku wakitumia ubunifu katika kuhudumia wageni wetu na kuzidi kukifanya chuo kujulikana kwa jamii hasa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na vyuo hivi karibuni”.
Tunawakaribisha watu wote kuja kusikiliza huduma zitolewazo na chuo na pia kujiunga na chuo hiki, katika maonesho hayo kuna wafanyakazi wa taasisi mbalimbali ambao wako maofisini na wangependa kujiendeleza kielimu wakiwa makazini hivyo chuo kipo hapa kuwasaidia kujiendeleza bila kuvuruga ratiba zao.

Naye Mkurugenzi wa OUT Kituo cha mkoa wa Dodoma Bw. Mohamed Msoroka, ameongeza kuwa tupo Katika maonesho haya kurahisisha kuwafikishia huduma jamii badala ya wateja kutufuata ofisini. Aidha, amewahimiza kutembelea banda la chuo kwa wingi ili kupata huduma za udahili, usajili na ushauri kuhusu programu mbalimbali zitolewazo na chuo.
Maonesho haya yamefunguliwa rasmi Agosti Mosi, 2024 na yanatarajiwa kufika kilele Agosti 8, 2024 katika Viwanja vya Nanenane jijini Dodoma. Tunawaalika na kuwakaribisha watu wote kutembelea banda la Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kuona fursa mbalimbali za kielimu zitolewazo na chuo hiki.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news