Rais Dkt.Mwinyi azidi kuwaheshimisha wanafunzi Zanzibar

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema,Serikali itaendelea kuwekeza zaidi katika sekta ya elimu kwa kujenga miundombinu bora na kuboresha maslahi ya walimu ili mafanikio yanayopatikana yaongezeke kila mwaka.
Amesema hayo Agosti 26,2024 katika viwanja vya Ikulu, Mjini Unguja, kwenye hafla maalum ya chakula cha mchana aliyowaandalia wanafunzi wa kidato cha nne na sita waliofanya vizuri katika mitihani yao ya taifa ya mwaka 2023 (kidato cha nne) na mwaka 2024 (kidato cha sita) kwa upande wa Unguja.
Rais Dkt. Mwinyi ameeleza kufarijika kwake na mafanikio yaliyopatikana, ikiwemo ongezeko la idadi ya wanafunzi waliopata daraja la kwanza.

Aidha, amesisitiza kuwa Serikali itaweka kipaumbele kuimarisha miundombinu, kuajiri walimu zaidi hasa kwa masomo ya sayansi, na kusimamia maslahi ya walimu ili kuwaongezea motisha ya kufanya kazi kwa ufanisi.
Rais Dkt. Mwinyi amefahamisha kuwa Serikali inakusudia kuongeza fedha za mikopo kwa ajili ya wanafunzi wa elimu ya juu, na ametoa wito kwa wanafunzi kutumia fursa hiyo kujiendeleza zaidi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news