Rais Dkt.Samia atoa maagizo kwa NHIF

DODOMA-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameutaka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), kuhakikisha wanawafikia wananchi wote ili wawe ndani ya mfumo wa Bima ya afya.
"Nataka bima kwa watu wangu wote, nitawaita tuzungumze," amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Ameyasema hayo leo wakati akitembelea maonesho ya Nane Nane kitaifa mkoani Dodoma.

Hivi karibuni Mhe. Rais akiwa ziarani mkoani Katavi na Rukwa kwa nyakati tofauti alihamasisha wananchi kukata bima ya afya ili wawe na uhakika wa kupata huduma za matibabu wakati wote.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news