Serikali inafanya kazi kupitia nyaraka-Mheshimiwa Sangu

NA VERONICA MWAFISI

NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu amesema kuwa msingi mkuu wa ufanyaji kazi wa Serikali ni kwa kupitia nyaraka ambazo zinaisaidia Serikali kutimiza uwajibikaji katika kutekeleza majukumu yake kupitia miongozo ya nyaraka hizo.
Naibu Waziri Sangu ameyasema hayo leo Agosti 28,2024 wakati wa ziara yake ya kikazi katika ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa iliyolenga kuhimiza uwajibikaji.
Naibu Waziri Sangu amesema kuwa utunzaji wa nyaraka kupitia Idara hiyo ni jukumu adhimu linalohitaji viwango vikubwa vya usimamizi ili kuleta haki na uwazi katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya Serikali kwa kutumia nyaraka hizo.

Aidha Mhe. Sangu ameipongeza Idara hiyo kwa namna wanavyofanya kazi kubwa ya kuwaenzi waasisi wa Taifa la Tanzania kwa kukusanya na kutunza kumbukumbu zao zitakazosaidia vizazi vijavyo kufahamu historia ya nchi kupitia waasisi hao.
Awali, Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa vibali vya ajira na kuwezesha idadi ya watumishi kuongezeka kila mwaka kwa lengo la kuongeza ufanisi. Naye, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bi. Editha Beda, wakati akitoa neno la shukrani amesema menejimenti imepokea maelekezo yote na kuahidi kuyafanyia kazi kwa ukamilifu ili kuongeza ufanisi katika utendajikazi kwa ustawi wa taifa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news