Serikali itaendelea kuwapa motisha wanafunzi-Rais Dkt.Mwinyi

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuwa Serikali itaendelea kuwapa motisha wanafunzi waliofanya vizuri kila mwaka kwa kuwapatia zawadi ya laptop na fedha taslimu.
Dkt. Mwinyi amesema hayo Agosti 22,2024, alipojumuika na wanafunzi wa kidato cha nne na cha sita kutoka skuli za Pemba waliofanya vizuri kwa ufaulu wa daraja la kwanza, katika hafla ya chakula cha mchana aliyowaandalia iliyofanyika Ikulu Pagali, Pemba.
Aidha, Dkt. Mwinyi ameahidi kuwafadhili wanafunzi sitini ngazi ya shahada ya kwanza waliofaulu kidato cha sita kwa daraja la kwanza kutoka Unguja na Pemba.

Aidha, Dkt. Mwinyi ameahidi kuwafadhili wanafunzi sitini waliofaulu kwa daraja la kwanza katika mtihani wa kidato cha sita kutoka Unguja na Pemba, ili kuendeleza masomo yao katika ngazi ya shahada ya kwanza.
Rais Dkt. Mwinyi alieleza kuwa Serikali itaendelea kuajiri walimu wa masomo ya sayansi na kuboresha maslahi ya walimu wote.

Halikadhalika, Dkt. Mwinyi amesema Serikali itajenga skuli za ghorofa za msingi na sekondari pamoja na kukarabati zile za zamani.

Vilevile, Serikali itaongeza fedha kila mwaka kusaidia udhamini wa wanafunzi wanaoendelea na masomo ya elimu ya juu.

Rais Dkt. Mwinyi amefahamisha kuwa ni mara ya kwanza Pemba kuweka historia kwa kuondosha daraja la sifuri katika matokeo ya kidato cha sita mwaka 2024.
Idadi ya wanafunzi waliopata ufaulu wa daraja la kwanza katika mtihani wa kidato cha nne ni 175, na kwa kidato cha sita ni 220, jumla ya wanafunzi 395 walihudhuria hafla maalum ya chakula cha mchana ambapo walitunukiwa zawadi ya heshima kwa kupewa Laptop ikiwa ni ishara ya juhudi na mafanikio makubwa waliyoonyesha.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news