Serikali itatoa fedha ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami wilayani Mbulu-Waziri Dkt.Nchemba

MANYARA-Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) amesema, Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami wilayani Mbulu Mkoa wa Manyara.Ameyasema hayo leo Agosti 23,2024 wakati akiwa mgeni rasmi katika Jubilee ya kutimiza miaka 25 ya Upadre ya Mhashamu Askofu Antony Gasper Lagwen wa Jimbo Katoliki Mbulu iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Bikira Maria Mpalizwa Mbinguni Mjini Mbulu mkoani Manyara.
Mheshimiwa Waziri ameahidi kuwa,Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 50 itakayojengwa kwa kiwango lami kutoka Hydom-Labay hadi Garbabi kuanzia robo ya kwanza ya mwaka huu wa fedha (2024/2025).

Barabara hiyo inatajiwa kugharimu shilingi bilioni 12 na itakapokamilika itarahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji wa abiria na mizigo kwa wakazi wa wilaya hiyo na Mkoa wa Manyara kwa ujumla.
Mhashamu Askofu Antony Gasper Lagwen, alizaliwa wilayani Mbulu mkoani Manyara mmwaka 1967 na alipata Upadre mnamo mwaka 1999 na baadae kuwa Askofu mwaka 2018.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news