SHINYANGA-Serikali kwa kushirikiana na Kampuni Williamson Diamond inaweka mikakati mbalimbali ya kukabiliana na changamoto ya kushuka kwa bei ya madini ya almasi katika soko la Dunia.

Hayo yalielezwa na Waziri wa Madini, Mhe.Anthony Mavunde wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya Mgodi wa uchimbaji na uzalishaji wa madini ya almasi katika mgodi wa Mwadui wa Williamson Diamond Ltd (WDL) mkoani Shinyanga.
Waziri Mavunde alisema kuwa, kwa sasa duniani kuna uhitaji wa madini mengine ambayo nayo yanahitajika katika sehemu mbalimbali duniani,hivyo kupelekea madini kuwa katika ushindani.
Waziri Mavunde alifafanua kuwa, Tanzania ni mwanachama wa Umoja wa Nchi zinazozalisha Almasi Afrika (ADPA), hivyo kupitia umoja huo nchi wazalishaji zimeendelea kujadili mikakati ili kurudisha thamani ya almasi katika masoko ya ununuzi na hasa katika kukabiliana na almasi ya maabara.
Kwa upande wake, Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Nishati na Madini,Mhe.Masache Kasaka aliupongeza mgodi kwa kazi nzuri inayofanywa na Menejimenti ya Uongozi wa mgodi.
Ni katika jitihada walizofanya za kukabiliana na athari kwa jamii pindi bwawa la kuhifadhi maji lilipopasuka na kuitaka Menejimenti ya Mgodi kusimamia na kutekeleza maelekezo yote yaliyotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ilipotembelea hapo.

Ni kwa kuwashirikisha na kuwasaidia namna bora ya kufanya uchimbaji bila kuathiri maeneo yanayozunguka mgodi hii itakuwa faida kwa mgodi na mkoa kwa ujumla.

Mwenda aliongeza kuwa, mgodi unauwezo wa kuendelea kuzalisha almasi kwa kipindi cha miaka hamsini ijayo hii ni kutokana na makadirio ya mashapo yaliyopo mgodini.