Serikali yadhamiria kurejesha Morogoro ya viwanda

MOROGORO-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa Serikali imejipanga kurejesha ile hadhi ya kihistoria ya Mkoa wa Morogoro kuwa mkoa wa viwanda kwa kufufua viwanda na kuvutia uwekezaji mpya.
Rais Dkt. Samia ameyasema hayo wakati akihutubia wakazi wa Mkoa wa Morogoro katika Uwanja wa Jamhuri akihitimisha ziara yake ya siku 5 kwenye mkoa huo.
Aidha, Rais Dkt. Samia amesisitiza kuwa uwepo wa miundombinu ya reli na uwepowa umeme wa uhakika kutoka Bwawa la Julius Nyerere unaufanya Mkoa wa Morogoro kuwa sehemu nzuri kwa uwekezaji.

Katika ziara yake Mkoani humo Rais Samia alitembelea uwekezaji wa upanuzi wa viwanda uliofanywa mkoani humo ikiwemo Kiwanda cha Sukari cha Mtibwa, na Kiwanda cha Sukari cha Kilombero.

Pamoja na mambo mengine, Rais Samia amesema kuwa upanuzi huo wa uwekezaji kwenye viwanda unampa imani kuwa ifikapo mwaka 2025/2026 Tanzania itakuwakatika
nafasi nzuri ya kujihakikishia uzalishaji wa sukari kukidhi mahitaji yake.
Rais Samia pia amesema kuwa uwezekaji huo na upanuzi wa viwanda vilivyopo niishara kuwa Tanzania ina mazingira bora na yanayovutia kwa uwekezaji wa viwanda.

Hivyo, ametoa rai kwa wakulima kuendelea kuzalisha kwa wingi ili kulisha viwanda vinavyojengwa.
Mapema leo, Rais Samia alizindua Kiwanda cha Sigara cha Serengeti (SCC) katika eneo la Kiwanda cha Uchakataji Tumbaku cha Mkwawa
(MTPL) ambapo amepongezi uwekezaji huo ambao utakamilika Juni 2025, na kuzalisha ajira mpya 12,000 mkoani Morogoro.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news