Serikali zote mbili zitaendelea kudumisha uhuru wa kuabudu-Rais Dkt.Mwinyi

DODOMA-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali zote mbili zitaendelea kudumisha uhuru wa kuabudu kwani ni njia muhimu ya kuimarisha umoja miongoni mwa Watanzania.
Rais Dkt. Mwinyi ameyesema hayo Agosti 15,2024, katika Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) uliofanyika katika Chuo cha Biblia cha Miyuji, Dodoma.Ameeleza kuwa,Serikali inathamini kazi zinazofanywa na taasisi za kidini nchini kwani zimekuwa msaada mkubwa kwa wananchi katika maeneo mbalimbali.

Wakati huo huo, Askofu Mkuu wa Kanisa la TAG, Barnabas Mtokambali, amemkabidhi Rais Dkt. Mwinyi Tuzo Maalum ya Uongozi Uliotukuka na kuthamini juhudi zake za kuimarisha uchumi wa Zanzibar.
Tuzo hiyo ni ya pili kutolewa na kanisa hilo tangu kuanzishwa kwake mwaka 1939.

Askofu Mkuu, Barnabas Mtokambali amempongeza Dk. Mwinyi kwa maendeleo makubwa yanayofikiwa na Zanzibar kwani yanaonesha dhamira ya dhati aliyonayo ya kuwatumikia wananchi.
Vile vile amezitaja sekta ambazo zinaipaisha Zanzibar kiuchumi kuwa ni Utalii, Uchumi wa Buluu, na Uwekezaji, Askofu Mkuu, Barnabas Mtokambali ameahidi kuwa kanisa hilo litaendelea kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Mara baada ya kumaliza mkutano huo, Rais Dk. Mwinyi alirejea Zanzibar na kupokelewa na viongozi mbalimbali wa Serikali na Chama Cha Mapinduzi, wakiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais, Mhe. Suleiman Hemed Abdallah, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news