TFRA yapongezwa kwa kuendesha Kampeni Kilimo ni Mbolea

MARA-Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evance Mtambi, ametoa pongezi kwa Wizara ya Kilimo na Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) kwa kuendesha kampeni ya "Kilimo ni Mbolea" yenye kauli mbiu "Ongeza Mavuno kwa Matumizi Sahihi ya Mbolea" iliyofanyika katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa Mashariki, hususan Simiyu na Mara.
Ameeleza kuwa, kampeni hiyo itaongeza uelewa na hamasa kwa wakulima katika kuongeza matumizi sahihi ya mbolea, jambo ambalo ni muhimu kwa kuongeza uzalishaji wa mazao kwenye eneo dogo na kuongeza tija kwa wakulima.
Ameongeza kuwa, matumizi ya mbolea katika mikoa hiyo bado yako chini ya asilimia 40, hivyo ameahidi kuwa Serikali za Mikoa husika zitafanya jitihada kuhakikisha wakulima wanajitokeza kusajiliwa ili kunufaika na mbolea za ruzuku zinazotolewa na serikali ya Rais, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu hassan.

Pia, amewasihi wananchi kujitokeza kuhuisha taarifa zao kwenye daftari la wapiga kura na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2024.
Kwa upande wake, Meneja wa TFRA wa Kanda ya Ziwa Bw. Michael Sanga amesema kuwa kampeni ya Kilimo ni Mbolea inalenga kuwaelimisha wakulima juu ya umuhimu wa matumizi sahihi ya mbolea ili kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao na kuwahamasisha kujisajili kwenye mfumo wa mbolea za ruzuku ili wapate pembejeo kwa gharama nafuu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news