Thierry Henry ajiuzulu France U-23

NA DIRAMAKINI

KOCHA Mkuu wa timu ya taifa ya Ufaransa chini ya miaka 21 (France U-23), Thierry Henry amejiuzulu huku taarifa ya Fédération Française de Football (FFF) ikitaja uamuzi huo ameufikia kwa sababu zake binafsi.
Thierry Henry amejiuzulu ukocha France U-23.(Picha na Getty Images).

Aidha, hayo yanajiri baada ya kocha huyo kuongoza timu hiyo kutwaa Medali ya Fedha katika mashindano ya Olimpiki 2024 yaliyohitimika hivi karibuni nchini Ufaransa.

Thierry Henry alipewa jukumu la kuiongoza timu hiyo Agosti 2023, akichukua nafasi ya Sylvain Riopun na alikuwa ametia saini mkataba wa miaka miwili hadi 2025.

Kupitia taarifa ya FFF, Thierry Henry alieleza kuwa, "Ningependa kuwashukuru FFF na rais (wa shirikisho) Philippe Diallo, ambao walinipa fursa hii nzuri.

"Kushinda Medali ya Fedha katika Michezo ya Olimpiki kwa nchi yangu kutasalia kuwa moja ya fahari kubwa maishani mwangu. Ninashukuru sana shirikisho, wachezaji, wafanyakazi na mashabiki walioniruhusu kuonesha uzoefu wangu." (NA)

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news