Watumishi wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko SUA wajengewa uwezo

MOROGORO-Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Menejimenti, Rasilimali Watu na Utawala, Bw. Peter Mwakiluma amehitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko kwa kuwataka kuwa na misingi ya utumishi bora kwa kuvaa mavazi nadhifu sambamba na kufika kazini kwa muda unaotakiwa.Bw. Mwakiluma amesema mtumishi wa umma hupimwa kwa nidhamu yake katika kuwahi kufika ofisini, mavazi anayo yavaa pamoja na kutekeleza majukumu husika.
"Inashangaza kuona mtumishi anachelewa kufika kazini lakini huyo huyo anataka muda wa kutoka atoke muda ule ule sasa jamani tutakuwa hatuwatendei haki wananchi," alisema Bw. Mwakiluma.
Katika mavazi amesisitiza kuwa mtumishi wa umma hutambulika kwa mavazi yake ambayo yapo kwenye msingi wake, akisema mavazi yenye maandishi hayatakiwi sambamba na kuvaa nguo zenye kuonesha sehemu kubwa ya mwili hayatakiwi.
Pamoja na kuhimiza hayo, Bw. Mwakiluma amempongeza Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko Bi. Suzana Magobeko kwa kuandaa mafunzo hayo kwani yatakuwa na mchango chanya katika utekelezaji wa majukumu kwa watumishi wa kitengo hicho.
Amesema,mafunzo kama hayo ni muhimu hata kwa vitengo vingine kwani yanaongeza ari mpya kwenye ufanyaji kazi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news