MOROGORO-Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Menejimenti, Rasilimali Watu na Utawala, Bw. Peter Mwakiluma amehitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko kwa kuwataka kuwa na misingi ya utumishi bora kwa kuvaa mavazi nadhifu sambamba na kufika kazini kwa muda unaotakiwa.
Bw. Mwakiluma amesema mtumishi wa umma hupimwa kwa nidhamu yake katika kuwahi kufika ofisini, mavazi anayo yavaa pamoja na kutekeleza majukumu husika.


