Wizara ya Madini yabainisha mikakati kupambana na magonjwa ambukizi migodini

DODOMA-Imeelezwa kwamba kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2022 hadi Agosti 2024 , Wizara ya Madini imeendelea kuratibu na kusimamia Masuala yanayohusu Usalama Mahali pa kazi pamoja na afya za wafanyakazi katika migodi ikiwemo UKIMWI , Kifua Kikuu na magonjwa sugu.
Hayo yamebainishwa Agosti 29, 2024 na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Wizara ya Madini, Festus Mbwilo kwa Kamati ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI.Mbwilo ameeleza kwamba, katika kipindi husika, Wizara iliratibu Upimaji wa Kifua Kikuu na magonjwa sugu yasiyo ambukiza ambapo jumla ya watu 396 walipima, kati ya hao 184 ni wafanyakazi na 212 ni jamii inayozunguka mgodi.
Akielezea kuhusu mkakati wa Wizara Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa amesema, Wizara inaendelea kusimamia na kuratibu utekelezaji wa mkakati wa masuala ya UKIMWI na magonjwa yasioambukizwa katika migodi mikubwa na ya Kati ili kupunguza maambukizi mapya na kuimarisha nguvu kazi ya wafanyakazi na jamii kama mkakati wa sekta ya madini unavyoelekeza kuhusu kudhibiti maambukizi ya UKIMWI, Kifua Kikuu na Magonjwa sugu.
Dkt.Kiruswa ameongeza kuwa, mkakati mwingine ni kushulika na vichochezi vya kijamii na kimfumo dhidi ya VVU kwa kutumia minutes za ushirikishwaji katika maeneo ya ndani na nje ya midogo sambamba na wachimbaji wadogo ambao wao wapo katika hatarishi zaidi kutokana uchimbaji wa kuhamahama.
Dkt.Kiruswa ameongeza kuwa, ili kuendelea kupambana na maambukizi ya VVU na magonjwa sugu, Wizara itaendelea kushirikiana na taasisi binafsi zinazoshughulika na afya kubuni mbinu mpya rafiki katika kutoa elimu ya afya na kuzikumbusha kampuni za uchimbaji madinib ziendelee kuchangia mfuko wa kupambana na maradhi.

Kwa upande wake , Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI , Bernadetha Mshashu ameipongeza Wizara ya Madini kwa kazi nzuri inayofanya ikiwa pamoja na kutekeleza maagizo yanayotolewa na Kamati kuhusiana na ujumuhishaji wa jamii ndani na nje ya migodi katika kutoa elimu ya afya.

Akizungumza kwa niaba mgodi wa Uchimbaji dhahabu Geita (GGM) Daktari Aalen Mtemi amesema, mgodi wa GGM unatambua umuhimu wa afya ya mfanyakazi mahali pa kazi hivyo katika kipindi husika imeweza kuchangia shilingi bilioni 1.75 katika Mifuko ya Kupambana na Maradhi yasioambukizwa na yanayoambukizwa.
Naye, Mwenyekiti kutoka Chama cha Wachimbaji Wanawake Mirerani, Recho Njau ameishukuru Wizara ya Madini kupitia Tume ya Madini kwa jinsi inavyotoa huduma za afya kupitia Mamlaka za afya kwa wachimbaji wadogo Mirerani ikiwa pamoja na kutoa elimu ya afya kuhusiana na magonjwa yanayotokana na shughuli za uchimbaji madini ikiwemo Kifua Kikuu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news