Ziara ya Waziri Mavunde yaleta faraja kwa wachimbaji wadogo Lemishuko wilayani Simanjiro

MANYARA-Waziri wa Madini,Mhe. Anthony Mavunde amefanya ziara kukagua shughuli za uchimbaji madini na kusikiliza changamoto za wachimbaji wadogo katika eneo la Lemishuku wilayani Simanjiro, eneo ambalo ni maarufu kwa uchimbaji wa madini vito ya Green Garnet.Waziri Mavunde amepata nafasi ya kukagua uwekezaji uliofanywa katika uchimbaji wa madini katika Kijiji cha Lemishuku na kuahidi kwamba Serikali itafanikisha urushwaji wa ndege nyuki (drone) katika eneo hilo kwa ajili ya utafiti wa kina ili kuwaongoza vizuri wachimbaji wadogo.
Ni ili kuondokana na uchimbaji wa kubahatisha na kuongeza kuwa, mwishoni mwa mwezi Desemba, 2024 jengo la kituo cha ununuzi wa Madini litakuwa limekamilika ili kufanikisha urahisi wa biashara ya madini.

Aidha,Waziri Mavunde alieleza kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itatatuwa changamoto zote za Maji,Umeme,Barabara na Zahanati ili kuchochea shughuli za ukuaji wa sekta ya madini.

Katika ujenzi wa zahanati aliongoza harambee ambayo jumla ya matofali 4,500,saruji mifuko 183 na fedha shilingi milioni 23 zimepatikana.
Akitoa salamu zake Mbunge wa Simanjiro,Mh. Christopher Ole Sendeka, amemshukuru Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa ya kuboresha huduma za kijamii katika eneo hilo la uchimbaji na kumshukuru Waziri Mavunde kwa kuwa Waziri wa kwanza kufika katika eneo hilo kusikiliza na kutatua kero za wachimbaji.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Wadogo (FEMATA),John Bina na Mwenyekiti wa Mabroka Tanzania (CHAMATA),Jeremiah Kituyo wameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Madini kwa mipango ya uendelezaji wa sekta ya madini na kusisitiza kwa wachimbaji wadogo kuzingatia sheria za nchi.

Pia kwa wafanyabiashara wa madini kuhakikisha wanakata leseni ya biashara ya madini ili kuepuka usumbufu usio wa lazima. Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro,Mheshimiwa Fakhi Lulandala amewahakikishia wachimbaji wadogo wa eneo la Lemishuku kwamba Serikali ya ngazi ya wilaya kupitia taasisi mbalimbali zilizopo hapo zitahakikisha zinasimamia kwa ukaribu utekelezaji wa changamoto za wachimbaji ili kuweka mazingira mazuri ya uchimbaji katika eneo la Lemishuku.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news