SINGIDA-Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeibuka mshindi wa kwanza katika kundi la Taasisi za Fedha zilizoshiriki Maonesho ya Saba ya Mifuko na Programu za Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, yaliyofanyika kuanzia tarehe 8 hadi 14 Septemba 2024 katika viwanja vya Bombadier mkoani Singida.

Pia, Dkt. Biteko alipata fursa ya kutembelea banda la Benki Kuu na kupewa maelezo ya kina kuhusu namna Benki Kuu inavyosimamia mifuko ya udhamini wa mikopo kwa niaba ya Serikali.
Mifuko hii ni pamoja na Mfuko wa Udhamini wa Mikopo ya Mauzo Nje ya Nchi (Export Credit Guarantee Scheme - ECGS) na Mfuko wa Udhamini wa Mikopo kwa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati (Small and Medium Enterprises Credit Guarantee Scheme - SME-CGS).