DART watakiwa kutimiza majukumu yao ipasavyo

DAR-Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba amewataka watumishi wa Wakala wa Mabasi yaendayo Haraka (DART) kuhakikisha wanatimiza majukumu kwa kufanya kazi kwa bidii na kwa ufanisi,kwani wakala huo ni taswira ya nchi katika sekta ya usafirishaji.
Mhe. Katimba ametoa maelekezo hayo alipokuwa akizungumza na watumishi wa wakala hiyo katika Ofisi za Wakala Ubungo Maji jijini Dar es Salaam alipofanya ziara ya kikazi.

Pia, amewasihi kufanya kazi kwa kuzingatia miongozo na sheria zilizopo,kwani watumiaji wa huduma za usafiri huo wa umma ni wananchi ambao wanatoka maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi.

“Wakala huu ni wakala muhimu sana na unabeba heshima kubwa sana ya nchi yetu kwa sababu tunajua Dar es Salaam ndio sura ya nchi na watu wote wakifika wanafikia Dar es Salaam.

"Kwa hiyo haya yaliyopo Dar es Salaam hasa huduma za msingi kama usafiri huu wa umma ndio yanajenga heshima ya nchi, hivyo tutimize majukumu yetu kwa viwango vinavyotakiwa,” amesema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news