Dhamira ya Rais Dkt.Samia ni kuona wananchi wananufaika na miradi katika maeneo yao-Naibu Waziri Kapinga

MTWARA-Waziri Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema kuwa dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha wananchi wananufaika na miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye maeneo yao.
Kapinga amesema hayo leo Septemba 09,2024 wilayani Mtwara Mkoa wa Mtwara wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini iliyolenga kukagua visima vya kuzalisha Gesi Asilia katika eneo la Mnazi Bay pamoja na miradi inayofanyika kwa manufaa ya jamii kutokana na uwepo wa gesi hiyo (CSR) ikiwemo ujenzi wa kituo cha Afya na kituo cha Polisi katika eneo la Msimbati.
"Yote haya mnayoyaona ni matunda ya kazi nzuri ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye anaonesha kwa vitendo jinsi anavyowajali kwa kuhakikikisha mnapata huduma bora kupitia miradi hii,"amesisitiza Kapinga.

Ameeleza kuwa lengo la ziara hiyo ya Kamati ya Bunge ni kujionea thamani ya miradi hiyo ambayo itanufaisha wananchi wa Msimbati, ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Naibu waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko aliyoyatoa Novemba 15, 2024 mara baada ya kutembelea eneo hilo na kuzungumza na wananchi.
Amesema ujenzi wa kituo cha Afya unatarajiwa kukamilika tarehe 30 Septemba, 2024 huku ujenzi wa Kituo cha Polisi nao ukiwa ukingoni.

Kapinga amesisitiza kuwa, Serikali ipo pamoja na wananchi katika kuhakikisha inawapelekea maendeleo.

Katika hatua nyingine, Kapinga amewaasa wananchi kushiriki kikamilifu katika uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa kwa kuanza kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news