Dkt.Biteko azihimiza nchi za Afrika kunadi Ajenda ya Nishati Safi

WINDHOEK-Naibu Waziri Mkuu na Waziri na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amezitaka nchi za Afrika kubuni na kutumia rasilimali na vyanzo mbalimbali vya nishati vilivyopo kuchochea maendeleo ya uchumi miongoni mwa nchi hizo.
DKt. Biteko amesema hayo Mjini Windhoek, Namibia wakati akihutubia Mkutano wa Kimataifa kuhusu Matumizi ya Hydrogen kwa ajili ya kuzalisha Nishati ya Umeme.

"Afrika inahitaji kuunganisha nguvu na kuweka mifumo na sera za kuwezesha Matumizi ya Teknolojia na mbadala kwa ajili ya kuleta maendeleo endelevu miongoni mwa nchi washiriki.”

Akitoa mfano wa Tanzania, Dkt. Biteko ameueleza Mkutano huo kuwa Tanzania iko katika utekelezaji mkakati wa upatikanaji wa nishati ya uhakika kwa gharama nafuu na hivyo kuchochea maendeleo ya watu na taifa kwa ujumla.

Aidha, Dkt. Biteko amezitaka nchi hizo za Afrika kuifanya ajenda ya nishati safi kuwa ya pamoja miongoni mwa nchi hizo ambayo inapunguza gharama za uedeshaji na kupungguza changamoto za kiafya.

Amesema,Tanzania kwa upande wake itaendelea kuwa kinara katika matumizi ya Nishati safi kwa kushirikiana na mataifa mengine ya Afrika katika kupitia mifumo, miundo sera na sheria zinazolenga katika maendeleo endelevu, pamoja na changamoto za kifedha, miundombinu na masoko katika matumizi ya Hydrogen, lakini ushirikiano na uhusiano mzuri miongoni mwa nchi za Afrika linaweza kuwa suluhisho.

Awali, Mkutano huo ulifunguliwa na Makamu wa Rais wa Nchi hiyo, Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah ambaye aliwataka washiriki kutumia fursa ya mkutano huo kuanisha mbinu na mkakati unaoweza kutumika kuleta maendeleo ya nchi husika kwa kutumia rasilimali zilizopo.

Mhe. Netumbo amesema Namibia inajivunia matumizi ya Hydrogen kwa matumizi ya viwanda kwa manufaa nchi hiyo, nchi Jirani pamoja na mataifa mengine yaliyo katika mlengo wa matumizi ya nishati hiyo.

“Tanzania iko katika hatua za awali katika kuendeleza matumzi ya Hydrogen hivyo inatumia fursa ya Mkutano huo kujifunza kuhusu fursa na Changamoto zinazoweza kujitokeza.”

Nchi za Afrika ambazo ziko katika matumizi ya Hydrogen ni pamoja na Namibia, Afrika Kusini, Kenya, Maouritania na Morocco.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news