FCS yaandaa mpango wa kuzinusuru AZAKI kiuchumi

ARUSHA-Shirika la Foundation for Civil Society (FCS limeandaa mpango kazi utakaosaidia AZAKi kujikwamua kiuchumi kutokana na ushirikano utakaozikutanisha pamoja na Sekta Binafsi katika utekelezaji wa shughuli zao mbalimbali za maendeleo katika jamii.
Afisa Oparesheni na rasilimali watu wa FCS, Karin Mbaga Rupia, akizungumza wakati wa warsha maalum iliyoandaliwa na Shirika hilo kwa kushirikiana na Sekta Binafsi katika maadhimisho ya Wiki ya AZAKi inayoendelea jijini Arusha.

Hayo yamebainishwa na Afisa Oparesheni na rasilimali watu wa FCS, Karin Mbaga Rupia wakati wa warsha maalum iliyofanyika jijini Arusha katika maadhimisho ya Wiki ya AZAKi inayoendelea jijini humo.
Karin amesema kuwa, mpango kazi huo utakuwa mbadala wa AZAKi kujipatia fedha za kutekeleza miradi yake katika kuisaidia jamii, na kuboresha uhusiano mzuri kati ya AZAKi na Sekta Binafsi na Mashirika ya umma.
“Kwa zaidi ya miaka ishirini ya uzoefu wetu wa kufanya kazi na Asasi ndogondogo za kiraia kote nchini tumekuwa tukitoa ruzuku, kwa Asasi hizo, lakini kadiri siku zinavyosonga mbele uwezo wetu wa kifedha unazidi kupungua kutokana na mataifa ya nje tuliyokuwa tukiyategemea kwa msadaa wa kifedha kupunguza nguvu kutokana na athari za kiuchumi zinazoikumba Dunia.
"Hivyo tumebaini njia mbadala ya kujiimarisha kiuchumi ni kufanya kazi kwa kushirikiana na Sekta Binafsi na mashirika ya umma,”amesema Karin.

Kwa upande wake mwezeshaji wa warsha hiyo, Sara Teri ameeleza kuwa,mpango kazi huo utazipa fursa AZAKi, Sekta Binafsi na Umma, kushirikiana kuleta maendeleo kwenye jamii.
Mwezeshaji wa warsha hiyo, Sara Teri akitoa ufafanuuzi wa baadhi ya mambo alipokwa akijibu maswali mbalimbali ya washiriki waliohudhuria katika warsha hiyo.

Ameongeza kuwa,hiyo ni hatua muhimu kwa AZAKI na Sekta Binafsi, nakwamba itasaidia kutatua athari za kimazingira na changamoto za maendeleo katika jamii.
Naye mdau wa AZAKi ambaye pia ni Mbunge mstaafu, Janeth Mbene amefurahishwa na mchakato huo na kusema kuwa ili Taifa lipige hatua zaidi kimaendeleo na kufanikisha Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 hakuna budi Asasi za Kiraia, Sekta Binafsi na Umma kuwa kitu kimoja katika kila hatua kwa maslahi mapana ya jamii na Taifa kwa ujumla.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news