Hongereni JKT Ruvu kwa kujenga uchumi-RC Kunenge

PWANI-Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amelipongeza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Kikosi cha Ruvu kwa juhudi za kuchangia maendeleo ya sekta ya uchumi.
Kunenge ametoa pongezi hizo Septemba 4,2024 aliposhiriki sherehe za kuhitimu mafunzo ya vijana Operesheni miaka 60 ya Muungano Kikosi cha Ruvu, ambazo zilifanyika katika viwanja vya kambi hiyo wilayani Kibaha, mkoani Pwani.
Katika hotuba yake, Kunenge amesifu jeshi hilo kwa mchango wake katika jamii kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo.

Aidha, Kunenge aliomba Jeshi hilo kuendelea kuanzisha na kubuni miradi mipya, ikiwemo mradi wa bustani ya wanyamapori (Zoo) ambayo imekuwa kivutio kikubwa kwa watalii wa ndani na nje ya nchi.
Vilevile, ameutaka uongozi wa Jeshi hilo kushirikiana na serikali ya wilaya katika kuanzisha ranchi ndogo itaongeza uzalishaji na kipato kwa wananchi wa mkoa wa Pwani.

Katika hatua nyingine, Kunenge ameshauri Jeshi hilo kushirikiana na taasisi kama TARURA ili kuboresha miundombinu ya barabara, jambo ambalo litachangia kuongeza mapato ya mkoa.Kwa upande wake, Kamanda wa Kikosi cha 832 cha JKT Ruvu, Kanali Peter Elias Mnyani, amemshukuru kwa ushirikiano uliotolewa na taasisi mbalimbali mkoani Pwani wakati wa hatua za awali za vijana hao kujiunga na jeshi.

“Nimepata ushirikiano mkubwa kutoka RITA na NIDA katika hatua za awali za kujiunga kwa vijana,” amesema Kamanda Mnyani.
Aidha, amesema mafunzo hayo yamewajengea vijana uwezo wa kujiamini, ukakamavu, uzalendo, kujituma, upendo, umoja, na mshikamano.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news