ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dkt. Hussein Ali Mwinyi amezishauri taasisi za dini kushirikiana na taasisi za Serikali na binafsi kukemea maovu yote ndani ya jamii.

Aidha, Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa, suala hilo sio la kuachiwa taasisi au mtu mmoja bali ni wajibu kushirikiana kukabiliana na maovu hayo kwa pamoja.
